Wednesday, January 16, 2019

Je, ni wakati gani mwanamke mjamzito anatakiwa kuacha kufanya mapenzi?

Je, ni wakati gani mwanamke mjamzito anatakiwa kuacha kufanya mapenzi?
Ijapokuwa wapo wanawake wengi ambao wanaweza kabisa kuendelea kufurahia kufanywa hadi siku wanakwenda kujifungua , kuna baadhi ya nyakati mshauri wako wa afya anaweza kukushauri kuacha ngono kutokana na moja au yote kati ya yafuatayo:


  • umekuwa na tatizo la kujifungua kabla ya muda muafaka kabla ya ujauzito ulio nao
  • umetokewa na tatizo la kutokwa na damu kwenye uke
  • umekuwa ukitokwa na ute fulani ambao wataalamu wanauita kwa jina la "amniotic fluid"
  • umekuwa na tatizo la kwenye mlango wa uzazi, ambalo kitaalamu linajulikana kama cervical incompetence
  • kondo la nyuma limesambaa na kuziba kabisa mlango wa uzazi na kuanza kujitokeza kwa nje (placenta previa)