Wednesday, January 16, 2019

Mwanamke mmoja kati ya watatu hutazama video za ngono mara moja kwa wiki - utafiti

Mwanamke mmoja kati ya watatu hutazama video za ngono mara moja kwa wiki - utafiti
Sio wanaume pekee wanaopenda kuangalia video za ngono, utafiti uliofanywa nchini Uingereza umebaini kuwa mwanamke mmoja kati ya wanawake watatu wamekiri kuangalia video za ngono  walau mara moja kwa wiki. 

Na wengi wamedai kuwa huziangalia kwa kutumia simu za mkononi. Mpiga picha wa Uingereza, Amanda De Cadenet aliungana na Marie Claire kufanya utafiti kwa wanawake wa kisasa na uhusiano wao na video za ngono na kubaini kuwa wengi wao ni watazamaji wazuri na tena huangalia wakiwa peke yao, kwa raha zao, kuliko wakiwa wenzao wao.

Amanda alisema wanawake wengi walidai kuangalia video za ngono ili kujifunza vitu vya kuwaridhisha wapenzi wao ama wao wenyewe. Asilimia 70 ya wanawake waliofanyiwa utafiti walikuwa na umri kuanzia miaka 18 hadi 34.