Thursday, April 4, 2019

Mambo gani unapaswa kumfanyia mpenzi wako Kila siku? soma hapa

Mambo gani unapaswa kumfanyia mpenzi wako Kila siku? soma hapa
1. Mwambie mpenzi wako kiasi gani unavyompenda, sio kukaa kimya, atajuaje kwamba unampenda.

2. Mwambie 'Nakupenda sana' hata mara saba kwa siku, atajisikia furaha moyoni na hata kama alikuwa na wasiwasi na wewe sasa utakuwa wakati wakuamini kiasi gani unavyompenda.

3. Tumia angalau muda mchache wa kuwa nae sehemu tulivu mkipota vinywaji baridi na chakula, pia mtalazimika katika sehemu hiyo tulivu mjadili mipango yenu ya maisha, unaweza kutumia hata saa moja kwa mazungumzo au hata zaidi ya saa moja, sio unaenda dakika mbili unaondoka. Atakuona unakuja kumsanifu au unamuwahi mwingine, kama una kazi ya muhimu mweleze taratibu kwamba una kazi, hatabisha kama ni muungwana. Atakusikiliza na mtapanga labda kukutana kesho utakapokuwa na nafasi, tena hakikisha unatafuta muda wa kuwa na mpenzio.

4. Mfanyie Surprise au kitu ambacho hakikutarajia akilini mwake. Unaweza kumletea zawadi nzuri sana, labda simu ya mkononi, nguo ya ndani, au kitu chochote ambacho unajua hakikuwa akilini mwake.

5. Kama mnaishi pamoja, mnapoamka asubuhi unatakiwa umkumbatie mpenzio, mkeo au mumeo. Unaweza kumsifu kwa kazi ya jana ambayo kwa kiasi kikubwa uliifurahia, usimbanie kuhusu suala la kumsifia. Mpe moyo kwamba anayaweza mashamsham ya gadoro, au vipi? mpenzi msomaji.