Monday, December 16, 2019

Mwanamke anayefika kileleni mara 90 kila saa (+Picha)

Mwanamke anayefika kileleni mara 90 kila saa (+Picha) 
Mwanamke anayeingia kileleni mara 90 kila saa moja, amezungumza jinsi tatizo hilo nadra lilivyoyafanya maisha yake magumu kama jehanamu.

Cara Anaya anasumbuliwa na tatizo liitwalo ‘Persistent Genital Arousal Disorder’. Mwanamke huyo mwenye miaka 30, mkazi wa Arizona, Marekani, alikutwa na tatizo hilo lisilotibika miaka mitatu iliyopita na hupata mshindo wa mapenzi hadi masaa sita kila siku.
Lakini hata hivyo kile kinachofahamika kama kitu cha starehe zaidi kwa wanawake, kimegeuka kuwa mateso kwake.

Cara, anayeishi na mume wake Tony Carlisi, 34, na mtoto wao Merrick, 10, anasema: “Inafedhehesha, inachanganya, inaabisha. Unapokuwa karibu na watoto unajisikia kama shangingi sababu ya hisia hizi za nguvu zinavyoshambulia mwili kwa wakati mmoja.”
Hali hiyo imemfanya Cara aache kazi na kuwa mama wa nyumbani tu kuogopa kuaibika. Cara anadai kuwa hali hiyo ilitokea tu ghafla wakati akifanya shopping.

Wakati akitembea kwenye duka hilo alijikuta akisisimuka kwa kila kitu alichokiona au kukishika.
Bila kujua kinachoendelea, Cara aliendelea kupata hisia hizo hadi alipoanguka sakafuni na kufika kileleni mara kadhaa.
Akiwa na woga, Cara alijivuta hadi kwenye gari na kumpigia simu rafiki yake Jenny alipofika nyumbani na akishindwa kufafanua kilichotokea na aliendelea kufika kileleni jioni hiyo.
Baada ya kufika kileleni mara 160 katika masaa mawili peke yake, Cara aliamua kuvunja ukimya na kwenda hospitali ambako hakupata msaada wowote. Madhara ya hali hiyo ni pamoja na kupungukiwa maji, kuumia magoti na viwiko na kuchoka kwa kiasi kikubwa kutokana na kukosa usingizi.