Tuesday, December 17, 2019

Hiki ndio kiwango sahihi cha kupishana umri kati ya wachumba wanao-tarajia kuoana

Kwa Wanamme
Inashauriwa kwamba kwa mwanaume miaka 5 hadi 10 inafaa kupishana na mwanamke anayetarajia kumuoa. Kwa maana ya kwamba mwanaume anaweza kuoa mwanamke ambaye yeye mwanaume anakuwa amemzidi huyo mwanamke miaka miwili, 5 hadi 10, Kwa mujibu wa tafiti za wataalamu hiyo ni sawa.

Kwa Wanawake.
Inashauriwa pia kwa mwanamke kuzidi miaka 2 hadi miaka 5 kwa mwanaume anayetarajia kuolewa naye. Hii inamaanisha kwamba mwanamke akimzidi mchumba wake au mume wake miaka miwili hadi mitano itakuwa ni sawa hakutakuwa na tofauti kubwa sana wala madhara makubwa.

Kuna Athari kwa wanandoa wakipishaza zaidi ya miaka 10.
Wanandoa wanapokuwa wamepishana kwa zaidi ya miaka 10 kunakuwa na utafauti mkubwa katika kuhusiana kwao kama jinsi tulivyokwisha elezea.

Ushauri Kwa Wachumba Waliopishana Umri Mkubwa
Wachumba ambao wana tofauti kubwa ya umri wao, wanashauriwa kutafuta ushauri kwawashauri wazuri (good counselors) kabla ya kuoana.