Friday, April 5, 2019

Dalili za kutambua kama mtoto anatumika kingono

Dalili za kutambua kama mtoto anatumika kingono

Mdau amewasilisha baadhi ya hoja akizungumzia dalili ambazo zinaweza kuwa taarifa kama mtoto anatumika kingono. Hoja zake ni;

Mtoto kupata shida wakati wa kukaa au kutembea (miaka 2 - 10) na kuwaogopa baadhi ya watu kupita kiasi au sehemu fulani au vitu (miaka 0-5)

Mtoto kupenda kujishika sehemu za siri kiasi cha kujisahau mpaka kulala akiwa anajishika na kukaa chooni muda mrefu au kuhitaji kujisaidia mara kwa mara (miaka 0-5)

Anaweweseka usiku (miaka 0-5), anakataa/kusumbua kula au kutapika bila ugonjwa mahususi (miaka 0-5) na huona aibu na kujitenga (umri wote)

Hushindwa kuzuia haja kubwa (miaka 4-7), kuwa mkimya isivyo kawaida (umri wa balehe), kuwa na kiburi, maamuzi ya kukinzana na maagizo ( umri wa balehe) na kuwa na Msongo wa mawazo (8-17)

Je, wewe wafahamu nyingine? Tufahamishe